Nyumba , maisha au ndoa inakuwa nzuri ikiwa msingi wake ni
mzuri tu. Katika mmojawapo wa mifano yake, Yesu alisema habari ya watu
wawili-mtu mwenye akili aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba mgumu na mtu
mpumbavu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga. Upepo mkubwa ulipotokea,
mafuriko(maji) na pepo zikapiga nyumba hizo mbili. Ile iliypjengwa juu ya
mwamba mgumu ilibaki ikisimama, lakini ile iliyojengwa juu ya mchanga ilianguka
kwa anguko kubwa.
Yesu
hakuwa akiwafundisha watu namna ya kujenga nyumba. Alikuwa akikazia
uhitaji(lazima) wa kuweka maisha juu ya msingi nzuri. Akiwa mjumbe wa Mungu
alisema hivi: “Kila asikiaye hayo maneno yangu na kuyafanya”, anafanana na mtu
anayejenga juu ya mwamba. Lakini “kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye,”
anafanana na Yule anayejenga juu ya mchanga. –Mathayo 7:24-27
Fahamu
kwamba katika mifano hiyo miwili Yesu anaonyesha kwamba si kusikia tu shauri la
hekima na kujua tu jambo la kufanya. Kinachotofautisha kufanikiwa na kushindwa
ni kufanya shauri la hekima linavyosema. “Mkiyajua hayo, (wenye furahani) ninyi
mkiyatenda.” – Yohana 13:17.
Hivyo
ndivyo ndoa ilivyo. Tukiweka ndoa yetu juu ya msingi ulio kama mwamba,
itashinda mikazo ya maisha. Lakini msingi huo ulio mzuri unatoka wapi? Kwa
muumba wa ndoa, Yehova Mungu.Yeye alianza ndoa alipowaunganisha watu wawili wa
kwanza wawe mume na mke. Kisha akawapa maagizo ya hekima ili wapate faida.
Jambo ambalo lingeamua kama wangeishi milele ama sivyo, lingetegemea kufuata
maagizo hayo. Wote wawili waliyajua maagizo ya Mungu, lakini jambo la
kusikitisha ni kwamba waliruhusu choyo kiwazuie wasitii maongozi hayo.
Walichagua kutokufuata shauri hilo na, kwa sababu hiyo, ndoa na maisha yao
yaliharibika kama nyumba iliyojengwa juu ya mchanga.
Yehova
Mungu aliwaunganisha watu wawili wa kwanza katika ndoa, lakini yeye mwenyewe
hawafanyii watu waliooana mipango ya ndoa leo. Walakini, shauri lake juu ya
ndoa lingali linapatikana. Ni juu ya kila mtu leo anayejifikiria kuoa au
kuolewa aamue kama atafuata shauri hilo au hatalifuata. Vilevile neno la Mungu
linaonyesha kwamba tunaweza kumwomba atusaidie tuamue kwa hekima juu ya mtu
tunayetazamia kuoana naye. –Yakobo 1:5,6
Walakini,
hali zinatofautiana sana katika sehemu mbalimbali za dunia.Leo katika sehemu
nyingi za dunia, wanaume na wanawakewanajichagulia
wenyewe mtu wa kuoana naye. Lakini katika sehemu ya watu wanaoishi duniani leo,
watu wengi leo hujichagulia mabinti na vijana wa kuwaoa au kuolewa nao tena
hukutana nao Vyuoni, maofisini na hata barabarani. Katika sehemu nyingi za
dunia kijana anapata mke mara baada ya kulipishwa mahari tena kubwa jambo
ambalo sina hakika kama ni mpango wa Mungu, Ndipo kijana ujikakamua na tena kwa
sononeko moyoni ambalo baadae uja kuzaa manyanyaso kwa binti. Lakini hata hali
ziwe namna gani, Biblia imetoa shauri linaloweza kusaidia ndoa ifanikiwe kwa
muda mrefu.