Sunday, November 25, 2012

KUWEKEA NDOA YAKO MSINGI MZURI (2)





Photo: For the married ladies

Give your husband unconditional respect

Most women are willing to show respect to their husbands, but they want the man to act respectable first. They are willing to show respect, but want their men to be worthy of it. If a woman will learn to risk respecting her man when he is not perfect, he will open his heart to her and will become pliable to change. A man needs respect to feel safe enough to open up. When he feels he is being looked up to as the “head” in a relationship, he will automatically allow his wife to become the neck —she will be able to point her man in the right direction! Women generally have no idea how much sway they have over a man. The ancient Jewish proverb says, “The wise woman builds her house,” but “a disgraceful wife is like decay to his bones.” A wife is either building up or tearing him down her husband. 

By Mark Gungor
UJIJUE MWENYEWE KWANZA.
Wanataka nini katika ndoa? Mambo ya kimwili, ya moyoni  nay a kiroho unayotaka ni nini?
Ni mambo gani unayoona kuwa ya maana sana? Una miradi na njia gani za kuyatimizia? Ili ujibu maulizo hayo inakupasa ujijue mwenyewe. Jambo hilo si jepesi kama mtu anavyoweza kudhani. Linataka hekima ya hali ya juu ili tujichunguze, na hata hivyo haiwezekani kujijua mwenyewe kabisa katika kila jambo.Paulo mtume alionyesha jambo hilo alipoandika maneno haya katika  1 Wakorintho 4:4. “Maana sijui sababu ya kujishitaki nafsi yangu, lakini sihesabiwi haki kwa ajili hiyo; ila anihukumuye mimi ni Yehova.”
                Wakati Fulani muumba alitaka mwanadamu Ayubu ajue mambo Fulani aliyokuwa akikosa kuyafahamu, naye Mungu akamwambia hivi:  “Nitakuuliza neno, nawe niambie.” (Ayubu 38:30) Maulizo yanaweza kusaidia kujijua wenyewe na kupata kujua habari ya makusudi yetu. Basi jiulize mwenyewe upate kujua namna unavyopendezwa na ndoa.
                Je, wataka kuoa au kuolewa ili utimize mambo ya kimwili yanayotakiwa – chakula,mavazi,nyumba? Hayo ni mambo ya kwanza kwetu sote, kama biblia inavyosema: “Tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na vitu hivyo.” Na uhitaji wa ngono? Vilele hilo ni jambo la kawaida linalotakiwa. “Ni afadhali kuoa kuliko kuwaka tama.” (1 Timotheo 6:8; 1 Wakorintho 7:9) Je, kusudi la ndoa ni kuwa na mwenzi?. Hiyo ilikuwa sababu kubwa iliyomfanya Mungu aanzishe mpango wa ndoa. Sababu nyingine ilikuwa ya kwamba watu wawili washirikiane wafanye kazi pamoja(Mwanzo 2:18; 1:26-28) kutimiza kazi njema kunafurahisha na kunapaswa kuwe na thawabu yake: “Imempasa kila mtu ale na kunywa, aone mema kwa kazi yake yote ngumu. Hiyo ni zawadi kutoka kwa Mungu.” – Mhubiri 3:13.
                Watu wanaopendana wameuona moyo kwa muda mrefu kuwa mfano wa maoni yao. Lakini Biblia inauliza ulizo lenye kusumbua juu ya moyo: “Nani awezaye kuujua?” (Yeremia 17:9) Je! Unajua yaliyo katika moyo wako hakika?
                Mara nyingi, uzuri wan je unatuzuia tusijue mambo mengine ya moyoni tunayotaka. Unapotafuta mtu wa kuoana naye, je! Unataka sana kufahamika, kuonyeshwa fadhili na kuhurumiwa? Mambo ya kwanza ambayo sote tunataka ni haya: Mtu wa kuwa karibu nasi, wa kutumainia, wa kufunulia mambo yetu pasipo kuogopa kwamba atakasirika, mtu ambaye ‘hatakuzuilia huruma zake’. (1 Yohana 3: 17) Je! Unaweza kumpa mwenzi wako yote hayo, je! Naye atakurudishia yayo hayo?
                Yesu alisema: “Wenye furaha ni wale wanaoona uhitaji wao wa kiroho.” (Mathayo 5:3) Uhitaji wako wa kiroho ni nini? Je! Unahusiana na kutafuta kazi ya maisha? Utajiri? Mali za mwili? Basi, Je! Mambo hayo yanaleta amani na furaha ya moyoni? Kwa kawaida hayaleti. Kwa hiyo inatupasa tufahamu ya kwamba kunabaki na njaa ya roho ndani ya watu wote, hata yakiisha kutimizwa mahitaji yote ya kimwili. Roho yetu yatamani sana kujua kujua sisi ni nani, tuko namna gani, sababu ya kuwapo hapa, na tunakoelekea. Je! Wewe unaona uhitaji(ulazima) wa mambo haya ya kiroho, na namna ya kuyatimiza?

No comments:

Post a Comment