UJIJUE
MWENYEWE KWANZA.
Wanataka nini katika ndoa? Mambo ya kimwili, ya moyoni nay a kiroho unayotaka ni nini?
Ni mambo gani unayoona kuwa ya maana sana? Una miradi na
njia gani za kuyatimizia? Ili ujibu maulizo hayo inakupasa ujijue mwenyewe.
Jambo hilo si jepesi kama mtu anavyoweza kudhani. Linataka hekima ya hali ya
juu ili tujichunguze, na hata hivyo haiwezekani kujijua mwenyewe kabisa katika
kila jambo.Paulo mtume alionyesha jambo hilo alipoandika maneno haya
katika 1 Wakorintho 4:4. “Maana sijui
sababu ya kujishitaki nafsi yangu, lakini sihesabiwi haki kwa ajili hiyo; ila
anihukumuye mimi ni Yehova.”
Wakati Fulani
muumba alitaka mwanadamu Ayubu ajue mambo Fulani aliyokuwa akikosa kuyafahamu,
naye Mungu akamwambia hivi: “Nitakuuliza
neno, nawe niambie.” (Ayubu 38:30) Maulizo yanaweza kusaidia kujijua wenyewe na
kupata kujua habari ya makusudi yetu. Basi jiulize mwenyewe upate kujua namna
unavyopendezwa na ndoa.
Je,
wataka kuoa au kuolewa ili utimize mambo ya kimwili yanayotakiwa –
chakula,mavazi,nyumba? Hayo ni mambo ya kwanza kwetu sote, kama biblia
inavyosema: “Tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na vitu hivyo.” Na uhitaji
wa ngono? Vilele hilo ni jambo la kawaida linalotakiwa. “Ni afadhali kuoa
kuliko kuwaka tama.” (1 Timotheo 6:8; 1 Wakorintho 7:9) Je, kusudi la ndoa ni
kuwa na mwenzi?. Hiyo ilikuwa sababu kubwa iliyomfanya Mungu aanzishe mpango wa
ndoa. Sababu nyingine ilikuwa ya kwamba watu wawili washirikiane wafanye kazi
pamoja(Mwanzo 2:18; 1:26-28) kutimiza kazi njema kunafurahisha na kunapaswa
kuwe na thawabu yake: “Imempasa kila mtu ale na kunywa, aone mema kwa kazi yake
yote ngumu. Hiyo ni zawadi kutoka kwa Mungu.” – Mhubiri 3:13.
Watu
wanaopendana wameuona moyo kwa muda mrefu kuwa mfano wa maoni yao. Lakini
Biblia inauliza ulizo lenye kusumbua juu ya moyo: “Nani awezaye kuujua?”
(Yeremia 17:9) Je! Unajua yaliyo katika moyo wako hakika?
Mara
nyingi, uzuri wan je unatuzuia tusijue mambo mengine ya moyoni tunayotaka.
Unapotafuta mtu wa kuoana naye, je! Unataka sana kufahamika, kuonyeshwa fadhili
na kuhurumiwa? Mambo ya kwanza ambayo sote tunataka ni haya: Mtu wa kuwa karibu
nasi, wa kutumainia, wa kufunulia mambo yetu pasipo kuogopa kwamba atakasirika,
mtu ambaye ‘hatakuzuilia huruma zake’. (1 Yohana 3: 17) Je! Unaweza kumpa
mwenzi wako yote hayo, je! Naye atakurudishia yayo hayo?
Yesu
alisema: “Wenye furaha ni wale wanaoona uhitaji wao wa kiroho.” (Mathayo 5:3)
Uhitaji wako wa kiroho ni nini? Je! Unahusiana na kutafuta kazi ya maisha?
Utajiri? Mali za mwili? Basi, Je! Mambo hayo yanaleta amani na furaha ya
moyoni? Kwa kawaida hayaleti. Kwa hiyo inatupasa tufahamu ya kwamba kunabaki na
njaa ya roho ndani ya watu wote, hata yakiisha kutimizwa mahitaji yote ya
kimwili. Roho yetu yatamani sana kujua kujua sisi ni nani, tuko namna gani,
sababu ya kuwapo hapa, na tunakoelekea. Je! Wewe unaona uhitaji(ulazima) wa
mambo haya ya kiroho, na namna ya kuyatimiza?
No comments:
Post a Comment