LIPA
MADENI UNAYODAIWA.
1. Warumi
13:8-10 . Deni lipi tulilonalo?
-Deni
kubwa tulilonalo ni upendo.
“Msiwiwe
na mtu cho chote, isipokuwa kupendana; kwa maana ampendae mwenzake ameitimiza
sheria. Maana kule kusema, Usizini, Usiue, Usiibe, Usitamani; na ikiwapo amri
nyingine yo yote, inajumlishwa katika neno hili, ya kwamba, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Pendo halimfanyii jirani neno baya; basi
pendo ndilo utimilifu wa sheria”.
2. Mathayo
22:36-37. Upendo unaoneshwaje?
“Mwalimu,
katika torati ni amri ipi iliyo kuu? Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa
moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote”.
3. Yoeli 2:
15-16,17.
-Watu
wote wanatakiwa wamueshimu Mungu.
“Pigeni
tarumbeta katika sayuni, Takaseni saumu, kusanyeni kusanyiko kuu; Kusanyeni
watu, litakaseni kusanyiko, Kusanyeni wazee, kusanyeni watoto, Na hao wanyonyao
maziwa; Bwana arusi na atoke chumbani mwake, Na bibi arusi katika hema yake.
Hao makuhani, wahudumu wa Bwana, na walie kati ya patakatifu na madhabahu, Na waseme,
Uwaachilie watu wako, Ee Bwana, Wala usiutoe urithi wako upate aibu, hata
mataifa watawale juu yao;
Kwani waseme kati ya watu, Yuko wapi Mungu wao?”
4. 1 Timotheo
5:1
“Mzee usimkemee, bali umwonye kama
baba; na vijana kama ndugu;”
-Zama za mwalimu/ ujamaa mtoto alikuwa wa jamii yote
lakini hivi sasa mtoto ni wa familia peke yake na imefikia hatua mtoto amekuwa
ni wa mzazi mmoja ama baba au mama.
-Mtoto
asimami kwenye basi wakati mtu mzima au mzee anapoingia kwenye basi.
-Mzazi
wako akisha zeeka una wajibu wa kumtunza / kuwatunza.
-Wazee
hawafundishwi kwa maneno bali wanafundishwa kwa matendo hasa wale walio
watelekeza watoto wao wakati wa ujana.
5. Mithali
3:27-30
“Usiwanyime
watu mema yaliyo haki yao,
Ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda. Usimwambie jirani yako, Nenda,
urudi halafu, na kesho nitakupa; Nawe unacho kitu kile karibu nawe. Usiwaze
mabaya juu ya jirani yako, Ambaye ankaa karibu nawe na kujiona salama.
Usishindane na mtu bila sababu, Ikiwa hakukudhuru kwa lolote.”
-Watu
wengine wanawazungusha majirani wenye shida. Kama unacho na kipo karibu mpe
lakini kama hakipo mwambie hakipo kweli. Pia
usishindane na watu bali lipa ubaya kwa wema.
6. Mathayo
15:4-9.
“Kwa
kuwa Mungu alisema, Mheshimu baba yako na mama yako, na, Amtukanaye baba yake
na mama yake kufa na afe. Bali ninyi husema,
Atakayemwambia babaye au mamaye, Cho chote kikupasacho kusaidiwa na mimi ni
wakfu, basiu asimheshimu baba yake au mama yake. Mkalitangua neno la Mungu kwa
ajili ya mapokeo yenu. Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari
zenu, akisema, Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami. Nao waniabudu bure,
Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu.”
-Unapokataa
kuwasaidia wazazi wako huku ukisema ninaenda kumwabudu Mungu wafanya kazi bure.
Upendo ndio deni letu.
No comments:
Post a Comment