Sunday, October 28, 2012

TUNZA FAMILIA KWA KULIKABILI TATIZO LA VIJANA KABLA YA NDOA.





TUNZA FAMILIA KWA KULIKABILI TATIZO LA VIJANA KABLA YA NDOA.
                Siku hizi kuna mvurugiko, ufisadi mpya, mkandamizo wa jamii, kutoa mimba na magonjwa ya zinaa tele tele.
                Baba Fulani alishangaa kuona mabadiliko ya ya ghafla kwa binti yakeambaye alikuwa mchangamfu/mzungumzaji, sasa mwenye wasi wasi, pita pita nyingi huku akiwa amenuna. Hatimaye binti aliungama kuwa kijana wa kiume alimsihi kushirikiana naye kimwili(ngono).Baba yake alisema: “Nilijua kuwa mabinti wengine…………. Lakini siyo kwa binti yangu!”  Kosa liko wapi?
                Kilio hiki sasa kimewakumba wazazi wengi, mivuto ya ufisadi mpya imekaribisha mauti kwa vijana. Tunawezaje kuwasaidia vijana ambao wanazama katika bahari yenye mawimbi makubwa ya ufisadi kote duniani. Ebu soma Yeremia 25:32, Mathayo 24:38-39, Mwanzo 6:5.
                Tuwasaidieje vijana wetu?
                1.Tudumishe matengenezo kwa kumuitikia Mungu na kujali wajibu wetu, maana siku hizi watu wapo bize katika kutafuta fedha na kusahau kuwapatia malezi bora watoto wao. Ebu soma Malaki 4:5,6. Methali 22:6, Mwanzo 18:19.
                Tuwaandae watoto mapema sawa na kocha na wanariadha wake, tujiwekee program kabambe ya kuwaelimisha na umri wao, na wafundishwe kanuni za wanariadha wa kiroho mapema. 2 Timotheo 2:4,5; 1 Wakorintho 9:24,25.
-Kuza uhusiano wao na Mungu kwa mfano wako pia, yaani waone mfano wa mahusiano yako wewe mzazi na Mungu wako kwanza.
-Tuthamini neno la Mungu lisilokosea. Wafikie wakiwa bado kuvamiwa na dunia na falsafa za kupotosha.
-Wafanye watambue mahali wanapoweza kupata uwezo wa kushinda majaribu. Zaburi 119:9.
-Walinde vijana wako kwa bidii isiyokoma.
-Usimwachie mtu mwingine kazi hiyo, ifanye wewe mwenyewe.
-Usiwaachie majirani kumlea mtoto wako. Kutayarisha njia ukurasa wa 163-165.
Tunapaswa kufanya uchaguzi kati ya kupata vyote vya dunia hii na kukoswa watoto.
Hakuna mtu wa mbadala ya Baba/mama. Mafunzo hayo maalumu yalenge mathalani mkandamizo wa jamii, Mabadiliko ya ujinsia na majaribu yake.
Vile vile jibu maswali yao kwa busara bila kudanganya, Usiwaachie tu waalimu wa biolojia Shuleni, Waalimu wa mitaani wasimbabaishe.
Akiyakosa hayo kutatokea nini? Mathayo 5:20-22,27; Mithali 5:23; 22:8 Waeleze hadithi yote na matokeo yake.
                2.Dumisha wajibu uliopewa na Mungu wa Uongozi, Usiwaache wajiongoze wenyewe, Usiwe hafifu, Chekibobu. Eleza thamani ya zawadi ya uanariadha  1 Wakorintho 9:22-27 Uzima wa milele. Panua njozi zao za maisha ya baadae, Uwezo wa kuona kwa imani Waebrania 11:6, Zaburi 19:9-11 Waeleze juu ya ahadi za Mungu duniani na nchi mpya. Afya/kujibiwa sala/ndoa n.k . Waebrania 13:4, Warumi 1:8
                3.Wasaidie kumtafuta Mungu wao wenyewe. Walete kwa Yesu mapema Mathayo 19:13-15. Watie moyo kujifunza biblia, wafundishe kuomba. OMBA NAO.
                4.Watie moyo kutembea na marafiki wazuri na wakweli. Dunia yasema “Play safe” tumia mipira neno la Mungu jaribu tabia ”USIZINI” MADARASA YAFUNDISHAYO UJINSIA BILA KUTHAMINI LISEMAVYO NENO LA MUNGU NI HATARI. Methali 13:20; 1 Wakorintho 15:33. Kutayarisha njia ukurasa 181. Zaburi 1:1-2.
                5.Wape watoto shughuli za kufanya wasikae kizembe kizembe.Msemo wa zamani: “Shetani hutafuta kuitumia mikono isiyo na kazi” Watie moyo kushiriki mazoezi ya viungo.
                6.Wape wajibu wa kufanya na uone namna wanavyoendelea. Wafundishe kazi za kujitegemea mfano Bustani n.k . Uwe kando ukiwasaidia, ukiwatia moyo kuendelea mbele, Wasikilize, Gundua wanayopendezwa watie moyo wanapofanikiwa.
                7.Wapatie maburudisho yafaayo, weka katika maktaba vitabu vinavyofaa. Waelezee faida na hasara ya vitabu vizuri na vibaya.


No comments:

Post a Comment