WAUAJI WAKATILI
“Mikono yako ilinifanya ikanitengeneza , unifahamishe
ukanifahamishe nikajifunze maagizo yako” (Zaburi 119:73.)
Kiasi ni
matokeo ya kujitawala,pia kiasi inatusaidia kuweka mipaka kwa vitu fulani na
pia kutotenda kabisa vitu vingine.Tukirejea katika fungu letu hapo juu la
Zaburi 119:73 utaona mtunga Zaburi akimwuliza Mungu ampatie ufahamu.Ufahamu
utakaomwezesha Daudi kujifunza sheria za Mungu.
Sisi pia twaweza kumwomba Mungu kuhusu afya zetu ili
atusaidie kutii sheria kuhusu kiasi.Mungu alituumba hivyo anafahamu lililojema
kwetu kimwili,kiakili,na kiroho.
KUFANYA KUPITA KIASI
Soma
mafungu yafuatayo:- Mithali 20:13; Mhubiri 3:17; Mhubiri 12:12; Marko 4:19.
Zingatia jinsi kujitawala kunavyoelezewa labda utashangaa.
1.”Kula, Kunywa
au kulala kupita kiasi ni dhambi. Mwili na akili yenye afya huleta
furaha.”(Temperance, uk.138)
2.”Lazima tuwe na
kiasi kazini mwetu.....
”Kazi ya siku
isiendelee hadi usiku....Mungu amenionyesha kuwa watu ambaohuendelea na kazi
kwa muda mrefu sana hupoteza zaidi kuliko kufaidi. Huunguza nguvu zao, na
huendelea kutenda kazi wakitumia msituko wa Neva (nervous excitement).”
(Temperance,uk.139,140).
3.”Kujifunza kwa
muda mrefu ni sawa na kunywa kupita kiasi. Watu wajifunzao kupita kiasi
watakuwa na matatizo.” (Temperance, uk.140).
4.”Sababu
mojawapo ya afya mbovu kwa wanaume ni tamaa yao kuu kutaka wapate fedha .
Kusudi mahsusi kwa baadhi ya wanaume ni kupata fedha. Wanjinyima pumziko,
usingizi, na kila burudani nzuri maishani, ili kupata utajiri.” (Temperance,
uk. 140).
Watu wenye kupenda fedha wanafanyaje wanaposikia
ujumbe wa injili? Marko 4:19.
Watu watajwao katika Luka 12:16-21 na Luka
18:18-23 walikuwaje? Tamaa ya fedha ilitawalaje maisha yao? Habari zao
hutusaidiaje kuelewa Marko 4:19?
Wote wawili walifurahi kupata fedha
kiasi kwamba walipuuza hazina kubwa mno yaani uzima wa milelepamoja na Mwokozi.
Kutokuwa na kiasi kuliifungia nje injili isipenye mioyoni mwao na pia kuwazuia
kujenga tabia za kimbingu.
KULA KUPITA KIASI (Mithali 23:1,2,21).
Ni dhambi gani ya kawaida leo?
”Ulafi ni dhambi
iliyoenea sana siku hizi. Tamaa mbaya ya chakula hufanya wanaume kwa wanawake kuwa
watumwa. Kula kupita kiasi huzuia mtu kufikiri vizuri hivyo kumfanya asiweze
kufurahia ukweli wa neno la Mungu.” (Testimonies, Vol. 1, uk. 486).
Ulafi sio kutumia kujitawala.
Tunahitaji akili timamu ili kuelewa mapenzi ya Mungu katika maisha yetu. Ulafi
huathiri nguvu joto za watu kuliko kufanya kazi kupindukia. Chakula kisicho
hitajika huziba mishipa kwa sababu hakiwezi kutengenezwa nyama au damu. Chakula
kisichotumika ni mzigo kwa ini na hudhoofisha mwili. Counsel on Diet
uk.102,103.
Ni ushauri gani tuupatao kutoka katika Mithali
23:1,2,21? Je mlafi awezaje kuwa maskini?
Mithali 23:2 haisemi ujiue iwapo u
mlafi; bali hushauri umuhimu wa kujitawala. Mtunzi wa Mithali husisitizia kuwa
kula kupita kiasi ni tatizo baya, lazima tuwe waangalifu sana.
AKILI HAFIFU; MADAWA YA KILA SIKU
(Mithali 25:27; 1 Korintho 10:31).
Mithali 25:27 husema haifai kula asali nyingi
mno.Je ni neno gani la kisasa ambalo tungeweza kulitumia badala ya neno
”asali”?
Akili hafifu:Sukari husababisha chachu,na hii huifanya akili iwe hafifu na
mtu aharibikiwe. ”Mungu amenionyesha kuwa kiasi kikubwa cha sukari kina madhara
makubwa kuliko nyama.” (Counsels on Diet and Foods, uk 327,328).
Sukari nyingi mno huwa ni chanzo cha matatizo mengi ya kiafya. Utumiaji wa
sukari nyingi huleta matatizo katika uozaji wa meno. Sukari nyingi ( na mafuta mengi) huweza kuleta tatizo la
”uzito mkubwa”.Kufa katika umri mdogo huongezeka kadri unene unavyozidi mno.
Upo uhusiano pia kati ya sukari na ugonjwa wa kisukari. Mtu mwenye
uwezekano wa kupata ugonjwa wa kisukari aweza kuchelewa kupata ugonjwa huo kwa
kutumia chakula chenye wanga tele(nafaka isiyokobolewa) na sukari kidogo.
Na mwisho, sukari hudhoofisha chembechembe nyeupe za damu. Chembechembe
hizo ni muhimu kwa kuuwezesha mwili kupambana na magonjwa na vijidudu vya
maradhi.
Vileo vya kila siku: Je, kahawa, chai, baadhi ya
madawa ya kupunguza maumivu na vinywaji baridi; vyote kwa pamoja vimejaa nini?
Vyote kwa pamoja
vimejaa Kafein. Kafein ni dawa ya kulevya, hivyo itasababisha matatizo ya
kiafya. Kafein huleta ongezeko la sukari katika damu, ongezeko la msukumo wa
damu, na ongezeko la mapigo ya moyo. Kafein yaweza kusababisha vidonda vya
tumbo, na magonjwa ya moyo.
Kafein yaweza kumfanya mtu awe
mchangamfu sana au mnyonge aliyezubaa ajabu. Pia Kafein huweza kuleta madhara
kwa viumbe ambavyo havijazaliwa. Majaribio yaliyofanywa katika wanyama huonyesha kuwa Kafein nyingi husababisha
viumbe vichanga kuzaliwa vyenye mifupa dhaifu, kuzaliwa na uzito pungufu, au
kuzaliwa vimekufa.
Madhara ya Kafein huonekana kwa
kutumia tu kikombe kimoja hadi vitatu vya kahawa. Mtoto ndogo atumiapo chupa
moja tu ya soda yenye kKafein hupata madhara sawa na mtu mzima aliyetumia
vikombe vinne.
Ebu tafakari baada ya kusoma 1 Korintho 10:31.Je
kafein au sukari nyingi yaweza kuwa kikwazo katika ufahamu wako wa mambo ya
kiroho?
NI NANI ALIYE NA MACHO MEKUNDU?”
(Mithali 23:29-35)
Ni nini katika
nchi zinazoendelea na zilizoendelea kilicho chanzo cha asilimia 30 za wanaojinyonga;
chanzo cha asilimia 55 za ajali za
barabarani; Chanzo cha zaidi ya asilimia 60 za mateso kwa watoto; na chanzo cha
asilimia zaidi ya 80 ya ujambazi wote? Mithali 23:29-35. (Takwimu kutoka
Kathleen Whalen Fitzgerald,Alcoholism, [New York:Doubleday,
1988],uk.
Xii).
Chupa moja au mbili tu za pombe hufanya ubongo usiweze
kukusanya habari toka katika vitu viwili tofauti. Kiasi hicho cha pombe
hupunguza kukumbukumbu, kuona, ufahamu, na maamuzi. Pia huathiri utaratibu wa
mwili; kwa mfano:
1.Mfumo wa kinga: Pombe hupunguza
uwezo wa chembechembe nyeupe za damu kuweza kupambana na maradhi. Pombe
huongeza uwezekano wa kuugua kichomi, kifua kikuu, homa ya manjano, na kansa
mbalimbali.
2.Mfumo wa misisimko muhimu mwilini
(Endocrine system): Chupa mbili au tatu tu kwa siku huongeza uwezekano wa
kutoka mimba, kuzaa motto aliyekufa, au kuzaa mtoto asiyekomaa.
[Mfumo huu unayo viungo muhimu
(glands) ambavyo hutengeneza dawa maalumu (homones) ambazo husafirishwa na damu
kwenda zinakohitajika mwilini kusisimua utekelezaji wa kazi muhimu mwilini. Kwa
mfano Pancreas Gland (kongosho) hutoa dawa iitwayo Insulinambayo husisimua kazi
ya uyeyushaji wa wanga kuwa sukarirahisiifaayo kutumika mwilini. Pia ipo Gland
inayotoa madawa ya kusisimua kazi za uzazi mwilini; na kwa wanawake gland hiyo
(ovary) hutoa madawa ya Progesterone na Esterogen ambayo husisimua matendo
yanayohusika ili mama mjamzito apate kujifungua ipasavyo. Ulevi hudhuru
taratibu za mfumo huu.]
3.Mfumo wa mzunguko wa damu:
Kutumia pombe huongeza uwezekano wa ugonjwa wa moyo na hupunguza uwezekano wa
ugonjwa wa moyo na hupunguza kiasi cha sukari kihitajikacho damuni. Pombe
huongeza mafuta damuni na kuleta tatizo la msukumo mkali wa damu.
4.Mfumo wa usagaji wa chakula:
Pombe huvuruga tumbo na kusababisha vidonda vya tumbo. Na sehemu idhuriwayo mno
na pombe ni ini.
(Ini ni kiungo muhimu sana kwani huhusika kuharibu
sumu au vijidudu vibaya vivamiavyo mwili. Basi utumiapo kwa hiari vinywaji
vikali, unaongeza sumu na ini linapambana nazo, na lishindwapo kuzimudu lenyewe
hudhurika. Na baada tu ya muda wa masaa 8 hadi 24 baada ya ini kukoma kumudu
shughuli zake mtu hufa.
Mungu ameumba ini kwamba iwapo ni
sumu kidogo imelidhuru, basi ini linao uwezo kuunda chembechembe mpya kujijenga
upya, ila sumu iwapo imlivuruga lote, hasa kwa pombe kali, basi linakwama kwa
kudhuriwa na sumu kali, na mhusika huaga dunia).
Mambo ya Walawi
10:1-11 huthibitishaje kuwa kileo hudhuru uwezo wa mtu wa kufanya uamuzi?
Pombe na
vileo vikali hudhuru ubongo kiasi kwamba watu hushindwa kutofautisha kati ya
lililo sahihi na lililo kosa. Hawawezi kutofautisha kati ya lililo takatifu na
lililo ovu; lililo safi
na lililo najisi.
“Kutumia
vileo kuliwafanya wale wana wawili wa Haruni. Nadabu na Abihu, wachukue moto wa
kawaida walipoingia katika hema ya kukutania. Vijana hawa hawakuijua tofauti
iliyokuwepo kwani walikuwa wamelewa.” (SDABC,Vol.1, uk. 749).
LAKINI IMEANDIKWA KATIKA BIBLIA(Kumbukumbu la
Torati 14:22-26, 1Tmotheo 5:23).
Leo tunajifunza mafungu ya Biblia
ambayo Wakristo huyatumia kuhakikisha kuwa kutumia kileo kidogo si dhambi.
Neno ”divai” lilitumika kwa
Waebrania kuwakilisha kinywaji kitokanacho na zabibu zilizokamuliwa. Walitumia
neno ”yayin”.
Kinywaji hiki hakikuwa kileo. Lakini
kilipoachwa kwa muda mrefu kilichacha na kuwa kileo. (tukumbuke Agano la kale
liliandikwa kwa Kiebrania).
Katika agano jipya neno ”divai”
limetokana na neno la kiyunani, ”oinos”.
Ukumbuke kuwa Agano jipya lugha yake ya awali ni Kiyunani). Hapa pia ”oinos”
imetumika kuwakilisha kinywaji kitokanacho na zabibu zilizokamuliwa. Usomapo
Yohana 2:1-10
Yesu aliwanywesha watu katika harusi
ya Kana ya Galilaya kinywaji safi, kitamu, kisicholevya. Kimetajwa kuwa ni
”divai”.
Kumbukumbu
la Torati 14:22-26 huelezea jinsi makuhani walivyokuwa wanawaelekeza wana wa
Israeli kuandaa sikukuu ya mwaka ya mavuno wakati waletapo zaka kwa Mungu
kushukuruwema wake. Je unadhani kinywaji kilichotumika hapa ni pombe? La hasha,
watu wa Mungu hawangekuwa wanapokea rasmi mafundisho nyeti ya kiroho wakiwa
wamelewa.
Katika 1 Timotheo 5:23 Paulo
anampatia Timotheo ushauri kuwa atumie mvinyo kidogo kwa ajili ya tumbo lake.
Neno la kiyunani lililotumika pale ni ”oinos”. Neno lenye maana ya kinywaji
kilichotokana na kukamua zabibu. Swali litakuwa kama kinywaji hicho kilikuwa
safi au kiliachwa hadi kikachacha kiwe kileo?
Historia hueleza kuwa divai
isiyochacha, kinywaji safi cha mizabibu, kilitumika kama dawa. Aristotle(384-322BC),
Pliny(AD 24-79; mtu aliyeishi wakati mmoja na Paulo), na Athenaeus(AD 280);
kila mmoja wao kwa wakati wake huzungumzia matumizi ya kinywaji safi cha
mizabibu, yaani divai isiyochacha, kama dawa nzurikwa matatizo ya tumbo.
Kumbuka: Aliambiwa asitumie maji tu
bali mvinyo kidogo. Wengine leo huchukulia kama aliambiwa ”usitumie divai tamu ila tumia pombe kwa
ajili ya tumbo lako.” Je ushauri wa
Paulo katika 1 Timotheo 6:11,12 ungekuwa
wa busara gani iwapo kweli alikuwa anamshauri Timotheo kutumia pombe kama
dawa? (Kwa maelezo zaidi, soma ”Wine in
the Bible” kilichoandikwa na Samuele Bacchiocchi, na kucahapishwa na Biblical Perspectives,
4569 Lisa lane, Barren Springs, Michigan 49103).
NI MAGONJWA GANI YATOKANAYO NA UVUTAJI WA TUMBAKU?
Tumbaku hudhuru
kila sehemu ya mwili wa binadamu ambamo hugusa. Tangu kansa ya ulimi, mdomo,
mapafu, moyo, tumbo, ni muuaji namba moja. Tumbaku haisababishi kulewa, ila
inayo sumu kaliiitwayo ”Nikotini”. Nikotini huathiri ubongoni katika kipindi
cha sekunde saba. Hii ni mara mbili haraka zaidi kuliko muda utumiwao na sumu
ya sindano ya madawa ya kulevya (Heroin).
Biblia haiitaji tumbaku kwa vile
ilikuwa haioteshwi katika nyakati za Biblia. Unafikiri ni mafungu yapi katika
Biblia hutuagiza kuachana na uvutaji?
Ebu soma Ufunuo 22:14,15 angalia
neno ”wachawi”. Neno la kiyunani lililotumika hapa ni
”pharmakos”likimaanisha ”alishaye
wengine sumu”. Neno linalofanana na hilo ni
”pharmakon” linalomaanisha ”madawa ya kulevya”. Wachawi wa kale
walitumia madawa ya kalekulevya; na na iliandikwa katika Ufunuo 22:15 kuwa
watakuwa nje ya jiji la Yerusalemu mpya. Je watu leo wasisitizao matumizi ya
madawa ya kulevya(wachawi wa leo) hukumu yao itakuwaje mbele za Mungu?
HITIMISHO:Mungu alituumba, kwa hiyo tunaweza kumwomba atusaidi kufahamu kanuni zake za afya.Halafu tuzitumie kanuni hizi katika maisha yetu ili tuweze kuwa na dhamira safi kufahamu na kutenda mapenzi ya Mungu.
REJEA:
Ellen G
White,Counsels on Health, uk. 71,157,160(kuhusu ulafi); uk 81-90
(kuhusu tumbaku na madawa ya
kulevya);uk. 98-100 (kuhusu kutumia kadri tu na
Kiasi).
Ellen G White,Christ’s Object Lessons, Faida ambayo ni
Hasara, uk.252-259.
Ellen G White, The Desire of Ages, Umepunguk Sisi pia twaweza kumwomba Mungu kuhusu afya zetu ili
atusaidie kutii sheria kuhusu kiasi.Mungu alituumba hivyo anafahamu lililojema
kwetu kimwili,kiakili,na kiroho.
No comments:
Post a Comment